KESHO NI SIKU KUBWA KWETU
Written by Living Tarimo on June 8, 2023

“Mazingira ya michezo tunayocheza sasahivi naweza kusema ni mazingira ambayo hayapo kwenye ulimwengu wa mpira wa miguu lakini inabidi kujituma na ninaamini kesho tutakuwa na mchezo tofauti kutokana na mapumziko ya siku hizi mbili”
“Tumekuwa na Safari nyingi na mechi nyingi zenye huzuni na zenye furaha kwetu. Uchovu bado ni mkubwa kutokana na ratiba hii ngumu lakini mara zote tumekuwa tayari kupambana”
“Kesho ni mchezo wa mwisho wa ligi na ni sikukuu na siku kubwa kwetu ni siku ambayo tunaenda kusherekea mafanikio yetu kwa msimu huu na siku nzuri kuwa na mashabiki wetu” @officialcedrickaze